Mabata-maji ni ndege wakubwa wa maji wa jenasi Cygnus katika familia ya Anatidae. Wanaainishwa katika nusufamilia Anserinae pamoja na mabata bukini. Mabata-maji ni ndege wakubwa kabisa wa familia yao wenye shingo ndefu na domo pana. Spishi za nusudunia ya kaskazini zina rangi nyeupe tu, lakini spishi za nusudunia ya kusini ni nyeupe na nyeusi. Hula mimea ya maji hasa lakini manyasi mafupi na wadudu pia. Tago lao limejengwa kwa matete na mimea ya maji juu ya nchi kavu lakini karibu sana ya maji.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Bata-maji
Thumb
Bata-maji domo-fundo
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Anseriformes (Ndege kama bata)
Familia: Anatidae (Ndege walio na mnasaba na mabata)
Nusufamilia: Anserinae (Ndege wanaofanana na mabata bukini)
Vigors, 1825
Ngazi za chini

Jenasi 2, spishi 7:

  • Coscoroba Reichenbach, 1853
    • C. coscoroba (Molina, 1782)
  • Cygnus Bechstein, 1803
    • C. atratus (Latham, 1790)
    • C. buccinator Richardson, 1831
    • C. columbianus (Ord, 1815)
    • C. cygnus (Linnaeus, 1758)
    • C. melancoryphus (Molina, 1782)
    • C. olor (Gmelin, 1789)
Funga

Ndege hawa huzaana kwa kanda za kaskazini na kusini za dunia. Wakati wa majira ya baridi au ukavu huhama kanda za moto zaidi au ambapo mvua unanyesha. Spishi kadha, hususa Bata-maji Domo-fundo na Bata-maji Mweusi, zimewasilishwa nje ya eneo lao la usambazaji, k.m. Afrika ya Kusini.

Spishi za Afrika

  • Cygnus atratus, Bata-maji Mweusi (Black Swan) imewasilishwa katika Afrika ya Kusini
  • Cygnus olor, Bata-maji Domo-fundo (Mute Swan) inapatikana kwa kawaida katika Afrika ya Kaskazini, lakini imewasilishwa katika Afrika ya Kusini

Spishi za mabara mengine

Picha

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.