Nyege
From Wikipedia, the free encyclopedia
Nyege au ashiki ni uchu au hamu ya kujamiana ambayo hupatikana kwa wanaume na kwa wanawake. Neno hili la Kilatini hutumika hasa mtu alipo na kiwango kidogo cha nyege. Hapo ndipo utakaposikia kwamba fulani ana nyege kidogo ama mwanamume fulani amekosa nguvu za kiume. Hata hivyo, yafaa ijulikane kwamba kuna tofauti kati ya hamu ya ngono na nguvu za kiume. Mwanamume asiye na nguvu za kiume huenda akawa na kiasi cha nyege kinachofaa, lakini hawezi kujamiana na mwenziwe kwa njia inayofaa maana mwili wake hauitikii.