Aljeri
From Wikipedia, the free encyclopedia
Aljeri (Kiarabu: مدينة الجزائر, madīnat al-djazā'ir, "mji wa visiwa"; Kifaransa: Alger) ni mji mkuu pia mji mkubwa kabisa wa nchi ya Aljeria ikiwa na wakazi milioni 2 (mwaka 2005), pamoja na mitaa ya nje takriban milioni 5. Iko mwambaoni mwa bahari ya Mediteranea.
Aljeri ni makao ya serikali na kitovu cha uchumi, biashara, utamaduni na mawasiliano nchini.
Kasbah yake imeorodheshwa na UNESCO kama Urithi wa Dunia.