Mtaguso wa pili wa Nisea
From Wikipedia, the free encyclopedia
Mtaguso wa pili wa Nisea uliitishwa na malkia Irene wa Bizanti mwaka 787, ili kujadili matumizi ya picha takatifu na sanamu katika Ukristo, kutokana na ombi la Papa Adrian I (772-795).
Wakristo wengi wanauhesabu kuwa wa saba kati ya Mitaguso ya kiekumeni. Ni wa mwisho kufanyika wakati wa mababu wa Kanisa.