Farisi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Farisi (kwa Kigiriki: Περσεύς Perseus) ni shujaa katika hadithi za Mitholojia za Kiigiriki. Alitajwa kama mwanzilishi wa mji wa Mikene akiwa pia maarufu kwa kumuua dubwana Madusa. Katika masimulizi ya Wagiriki alitazamwa kama nusu-mungu, yaani mtoto wa mungu mkuu Zeu na wa binti wa kibinadamu Danaë. Alikumbukwa kuwa pamoja na mke wake Andromeda, binti mfalme wa Ethiopia, na wanao Perses, Alkaios, Sthenelos, Elektryon, na binti Gorgophone. Katika masimulizi hayo, Farisi pia ni babu-mkubwa wa Herakles.